Friday, October 19, 2012

UTOAJI WA MIMBA KWA WASANII WA BONGO MOVIE SASA NI KAMA MTINDO HURU” MAINDA…!!

UTOAJI wa mimba kwa wasanii wa bongo movie sasa ni kama mtindo huru kwani usipofanya hivyo unaweza kuonekana mshamba wa mji, ambapo msanii wa tasnia hiyo, Mainda, ametoa ushahidi wake kuwa aliwahi kumshudia mmoja wa mastaa wa tasnia hiyo akitoa mimba tena nyumbani kwake.

Msanii huyo alizungumza na mtandao wa
DarTalk, ambapo alidai kuwa wapo wasanii wengi wa tasnia hiyo ambao wanapata mimba lakini  walio wengi wanazitoa. Alisema kuwa kwa upande wa msanii huyo hawezi kumtaja kwani baada ya kufanya kitendo kile alimuomba asitoe habari hiyo, hivyo ana heshimu maombi yake ingawa ni kitu cha hatari kwani mara baada kumaliza alipoteza fahamu na alikuja kurudi katika hali yake baada ya masaa kadhaa.

Hata hivyo kwa upande wake alihisi kama ameigia kwenye shimo lenye wadudu wakali kwani endapo kama kuna kitu chochote kingetokea siku hiyo yeye angekuwa ni muhusika wa kwanza kuwajibishwa kwani hakukuwa na mtu mwingine zaidi yake.


“Si kitu cha ajabu kwa wasanii wa bongo movie kutoa mimba wapo wengi wanaofanya upuuzi huo wa hatari, wapo watu wengi ambao wameshapoteza maisha kwa sababu ya kujaribu kutoa mimba na wengine kushindwa kuzaa kabisa, lakini bado watu wanaendelea na ujinga huo,”
alidai.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...