Thursday, August 30, 2012

Warembo wanao wania tajhi la Redds Miss Kanda ya Mashariki 2012 wakiwa katika picha ya pamoja katika kambi yao uliyoanza jana  katika eneo la nane nane mnje kidogo ya mji wa Morogoro.

MAISHA PLUS 2012. BAADA YA LUSHOTO NI SANYAJUU,KILIMANARO

Awamu ya kwanza  ya zoezi la kwasaka vijana watakaoweza kumudu mchakamchaka wa shindano la Maisha Plus, imeanza jana
(Agosti 27) huko Bagamoyo mkoani Pwani.

Tuesday, August 28, 2012

SIKU chache baada ya kukanyaga ardhi ya Bongo kutoka uhamishoni nchini Kenya, nyota wa muziki wa kizazi kipya Afrika mashariki Rehema Charamila amesema kuwa hajarejea nchini kusaka wanaume.
Akizungumza juzikati jijini Dar Ray C amefunguka kuwa hakuja Tanzania kutafuta Bwana wa Kuolewa nae kama watu wanavyovumisha mitaani isipokuwa amefanya hivyo kwa ajiri ya mapumziko na kazi pia.
"Unajua mimi niliamua kuhamia Kenya baada ya kuona kuwa ninsupport kubwa kwa Mashabiki wa huko kuliko hapa Tanzania hivyo nikaamua kwenda kuwapa kile wanachokipenda na pia kujaribu kukuza muziki wangu, katika kusibitisha hilo hivi karibuni natarajia kuachia ngoma yangu mpya amabayo nimeipa jina 'Moyo Waniuma' alisema Ray…Sorce Teentz

ALIYE UWAWA MOROGORO,KATIKA MAANDAMANO YA CHADEMA 


Mtu mmoja anadaiwa kufa kwa kupigwa risasi Kichwani huku wengine kadhaa wakijeruhiwa vibaya kwa Risasi za moto baada ya Polisi kuwarushia Risaasi za moto na mabomu ya machozi waandamani wa Chadema mjini hapa.

Baadhi ya wafuasi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA mkoani Morogoro wakiongozwa na polisi baada ya kuwatawanyisha walipokuwa wakifanya maandamano maeneo ya Msamvu mjini Morogoro mchana wa leo. Polisi walitibua maandamano hayo yanayodaiwa kutokua rasmi kwa mabomu ya machozi.



Huyu ni Ally Zona muuza magazeti wa Msamvu Morogoro akiwa hajitambui baada ya kutandikwa risasi na Polisi kuzuia maandamano ya chadema
SOURCE -The choice


FIESTA 2012 ILINYOKUA TANGA

 FA & Linah ni Yalait au kunamengine???
  Wema,Aunt & Shilole...
  Shetta wa Darstamina kwa steji
Dj Zero kazini
CMB Prezzo 4rom Kenya Bhaaasss!
Nuru,Nuru,Nuru,Nuru Haaya.
Jb na Shilole

Monday, August 27, 2012

SIKILIZA WIMBO MPYA WA PAH ONE--ASAMBEENI 

JINSI FIESTA 2012 ILIVYOKUA MOSHI

Wasanii machachari Bongo Move Wema Sepetu (kushoto) na Aunt Ezekiel wakicheza muziki wa bongo Fleva uliokuwa ukishushwa na Msanii wa Bongofleva,Ferooz katika uzinduzi wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 Bhaaaaass! katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Mjini Moshi usiku huu. Tamasha hilo limebamba ile mbaya.

Ferooz akiwa na mmoja wa mashabiki wake wakilishambulia jukwaa vilivyo.

Sehemu ya wakazi wa mji wa Moshi wakiendelea kushuhudia makamuzi ya wasanii mbalimbali wanaotumbuiza usiku huu kwenye uzinduzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012.

Prezoo akiwarusha mashabiki kibao (hawapo pichani) waliojitokeza jioni ya leo kwenye uzinduzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012

CHINEDU IKEDIEZE(AKI) APATA MTOTO

AKI akiwa amembeba mtoto wake.
Nguli wa filamu nchini Nigeria Chinedu Ikedize alias AKI amefanikiwa kupata mtoto wa kike kutoka kwa mkewe Nneoma Hope Nwajah aliyejifungua siku kadhaa za nyuma nchini Nigeria.
Aki na mkewe huyo walifunga ndoa November 26 mwaka 2011 iliyofanyika nchini kwao na kuhudhuliwa na Celebrities kibao kutoka sehemu mbalimbali wakiwemo P-Square. Aki kwa sasa anaitwa baba akiwa na umri wa miaka 34.

Sunday, August 26, 2012

VIDEO YA MAN U(3) NA FULHAM(2)


TAZAMA VIDEO YA MAJEMBE CHELSEA vs NEWCASTLE 2-0

Saturday, August 25, 2012

NASIB ABDUL JUMAA KATIMBA KWA JAKAYA



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amemuita ikulu mwanamuziki anayefanya vizuri kwa sasa kwenye Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kumpa jukumu maalum,  Kwa mujibu wa Diamond
, juzikati ‘prezidenti’ alimwita ikulu Magogoni, Dar es Salaam na kumpa shavu la kwenda kufanya shoo kwenye mkutano maalum utakaofanyika Washington DC nchini Marekani hivi karibuni. “Yaa, rais aliniita akaniambia kuna shoo natakiwa kwenda kufanya Marekani. “Kwa mara ya kwanza nitasafiri nje ya nchi na madensa wangu wanne na msemaji mmoja. Sasa hivi hawataki kutembea na kupanda magari wasije wakakosa hiyo safari,” alisema Diamond na kuongeza kuwa baada ya kuumwa, mawazo aliyaweka kwenye mchongo huo hivyo mambo mengine yataendelea ikiwa ni pamoja na kufanya kolabo na mwanamuziki wa kimataifa wa Nigeria, J. Martins. Chanzo:www.globalpublishers.info


YANGA MPANGO MZIMA

Kikosi cha Yanga

Kiiza katika mechi 

Msuva katika kandanda
MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Yanga SC ya Dar es Salaam, wameanza vyema ziara yao ya mechi za kujipima nguvu nchini Rwanda
, baada ya jioni hii kuichapa Rayon Sport mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Amahoro mjini Kigali.

Yanga ambao jana walitembelea Ikulu ya Rwanda, walipoalikwa na rais Paul Kagame kupeleka Kombe la Afrika Mashariki na Kati, ambalo tangu mwaka 2002 mfadhili wake mkuu na mlezi wake ni Rais Kagame, mabao yake yalitiwa kimiani na Hamisi Kiiza dakika ya pili na Simon Msuva dakika 12.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb ameiambia BIN ZUBEIRY kwa simu kutoka Kigali kwamba, timu yao ilicheza vema na kuwazidi kabisa uwezo wenyeji wao na ilikuwa na uwezo wa kufunga mabao zaidi.

Bin Kleb alisema kwamba Yanga itashuka tena dimbani kumenyana na Polisi Jumapili na kwa mujibu wa ratiba ya awali, wanatakiwa kurejea Dar es Salaam Jumatatu.

Awali, Yanga ilikuwa icheze pia na mabingwa wengine wa zamani wa Kombe la Kagame, APR, lakini kutokana na timu hiyo kukabiliwa na mgogoro hivi sasa uliosababisha kufukuzwa kwa kocha Mholanzi, Ernest Brandy na nafasi yake kupewa kocha mzalendo kwa muda, imeshindwa kucheza.

Katika ziara hiyo, Yanga haijaambatana na mfungaji bora wa Kombe la Kagame, Said Bahanuzi ambaye amebaki Dar es Salaam kwa matatizo ya kifamilia. Yanga imekwenda Rwanda na msafara wa watu 42, wakiwemo wachezaji 28, Maofisa watano wa benchi la Ufundi na viongozi wanane.

Viongozi walio na timu Kigali ni Mwenyekiti, Yussuf Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini Mama Fatma Karume, Francis Kifukwe na Seif Ahmed ‘Magari’ sambamba na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Abdallah Bin-Kleb na Salum Rupia.

Yanga ilitwaa Kombe la Kagame kwa mara ya pili mfululizo wiki mbili zilizopita, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa kuifunga Azam FC mabao 2-0, ambayo yalitiwa kimiani na Hamisi Kiiza ‘Diego Milito’ na Said Bahanuzi ‘Spider Man’.

Hiyo kwa ujumla ilikuwa mara ya tano mfululizo, Yanga inatwaa Kombe hilo, baada ya awali kuchukua mwaka jana, wakiifunga Simba katika fainali bao 1-0, Uwanja wa Taifa mfungaji Kenneth Asamoah ambaye ametemwa, ingawa siku hiyo Kiiza pia alifunga bao safi, ambalo refa alilikataa.

Yanga ilichukua kwa mara ya kwanza Kombe hilo, mwaka 1975 ikiifunga tena Simba katika fainali, mabao 2-0 wafungaji Sunday Manara ‘Computer’ na Gibson Sembuli (sasa marehemu) Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Ikachukua tena mwaka 1993, Uwanja wa Nakivubo, Kampala, Uganda kwa kuifunga SC Villa mabao 2-1, yaliyotiwa kimiani na Said Nassor Mwamba ‘Kizota’ (sasa marehemu) na Edibily Jonas Lunyamila.

Ilichukua tena mwaka 1999, ikiifunga tena SC Villa, Uwanja wa Nakivubo, kwa penalti 5-3, kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120, Yanga ikisawazisha bao kupitia kwa Lunyamila, baada ya Hassan Mubiru kutangulia kuifungia Villa, siku hiyo Manyika Peter akicheza penalti mbili za Waganda.

Aidha, kwa kutwaa Kombe hilo chini ya Mbelgiji huyo, Yanga imeendeleza rekodi yake ya kutwaa mataji ya michuano hiyo, chini ya makocha wa kigeni baada ya mwaka 1975 kuchukua chini ya Tambwe Leya aliyekuwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kabla ya kuchukua uraia wa Tanzania, (sasa marehemu), 1993 chini ya Nzoyisaba Tauzany aliyekuwa raia wa Burundi kabla ya kuchukua uraia wa Tanzania, mwaka 1999 chini ya Raoul Shungu wa DRC na mwaka jana chini ya Mganda, Sam Timbe.
 Chanzo: Saleh Ally



Thursday, August 23, 2012

SHARO MILIONEA KAVUTA MKOKO M(15)


 Nani kasema kazi yakuchekesha hailipi? inalipa na ina soko kubwa sana. mkali wa comed na kuimba tanzania sharo milionea amenunua gari lenye thaman ya shilingi milioni 15 za kitanzania aina ya Opa.kama nyumba kaipata chata ya kitambulisho chake ya kuchekesha cha oooooh maaamaa!

ERIK OMONDI 

Erik Omond ni mchekeshaji mkubwa kutoka Nairobi Kenya,Bofya upate burudani ambayo itakuacha ukicheka sikunzima

Wednesday, August 22, 2012

Mwanamuziki anayelipwa pesa nyingi TZ, Diamond Platnums sasa anaonekana kwenye
Babkubwa Magazine mwezi huu






Friday, August 17, 2012

TAZAMA VALU VALU YA JOSE CHAMELEONE

BAADAE YA OMMY DMMPLOZ


DULLY 'MTOTO WA KARIAKOO' OFFICIAL VIDEO

KOFFII OLOMIDE ASHITAKIWA

Koffi Olomide, ambaye ni mwanamuziki mashuhuri barani Afrika ameshitakiwa kwa kumpiga Mtayarishaji wake wa muziki.
Mwanamuziki huyo alikamatwa na kufungiwa katika kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani jumatano.
Koffi alikamatwa kufuatia vurugu katika hoteli moja mjini Kinshasa.
Waandishi wa habari wanasema mahakama hiyo ya Kinishasa ilifurika kutokana na watu wengi kuja kumuona kiongozi huyo wa bendi ya Quartier Latin akiwa kizimbani.
Kesi hiyo iliharishwa hadi Alhamisi asubuhi wakati atakaposhitakiwa rasmi.
Wakati wa kesi hiyo hapo jana Koffi Olomide aliwakilishwa na mawakili 10.
Ugomvi kati ya mwanamuziki huyo na mtayarishi wake Bwana , Diego Lubaki, ni kuhusu pesa dola $3,680.
Hakimu alimfahamisha mwanamuziki huyo ikiwa atapatikana na hatia huenda akafungwa jela miezi sita.
Olomide ni gwiji wa muziki aina ya "soukous", mtindo ulitokana na jina la kifaransa "secouer", lenye maana ya kujitikisa au kujinengua ,na wachezaji wake vile vile wanatambulika kwa kunengua maungo.




Thursday, August 16, 2012

MWANAMKE TAJIRI NA MREMBO

JARIDA  maarufu la  Times nchini  Uganda  limemtaja mama wa watoto wawili Zari Hassan kuwa ndiye mwanamke mrembo na tajiri kuliko wote nchini humo kwa wakati huu.

Kwa  mujibu wa  jarida hilo Zari (30) ambaye ni Mwanamuziki,Mfanyabiashara na Mtangazaji wa  runinga  amepata mafanikio makubwa  kwenye  muziki na pia  kipindi chake cha runinga  kinachofananishwa na  kipindi cha ‘Keeping up with the Kardashians’ kinachoendeshwa na mrimbwende wa kimarekani Kim Kardashian.

Huku likiambatanisha picha za magari na  nyumba  anazomiliki mwanadada huyo, jarida hilo limeandika  kuwa  huenda akaingia kwenye orodha ya wanawake matajiri zaidi Afrika baada ya kipindi kifupi kijacho endapo ataendelea na mwenendo wake wa sasa kibiashara.
hata  hivyo jarida hilo pia  limetaja  zari kuwa mmoja wa mstaa wapenda…








Monday, August 13, 2012

Gazeti la DAILY POST limeandika kuwa mshahara atakaokuwa anapokea Prezzo ni dola 720,000 kwa mwaka akiwa balozi wa One Campaign.
Fedha hizo ni sawa na shilingi bilioni 1, milioni 137 na ushee za Tanzania!
Kwa mshahara huo Prezzo atakuwa akilipwa zaidi kuliko hata viongozi wakubwa Kenya.
Mshahara wa rais Mwai Kibaki ni shilingi za Kenya milioni 3.2 sawa na milioni 57 za Tanzania na waziri mkuu Raila Odinga akipokea milioni 2.4 za Kenya huku Uhuru Kenyatta akipokea kama milioni 1.5 kwa mwezi.
Hii ndo payslip ya Prezzo:
Mshahara kwa mwezi : $40,000 (TSH 63,200,000)

Posho ya nyumba : $5400 (TSH 8,532,000)

Posho ya usafiri : $6600 (TSH 10,428,000)

Kuburudika: $5000 (TSH 7,900,000)

Matibabu: $10,000 (TSH 15.800,000)
Vingine: Passport ya kidiplomasia na…






Growing up i always loved to play dressup which brings me down to the why i do what i do. To me fashion is about taking risks, trying new things, putting together different pieces, patterns and styles to finally produce a fascinating look. Styles change but with a good fashion taste you will always be trending.
Sachques collections/fashions aims at instilling that daring knowledge in women by providing them with most currently favoured styles of attires to fit…


Friday, August 10, 2012

Ndio, ni kweli !! Mwanamuziki huyu mkubwa wa Pop duniani ataongea moja kwa moja na wewe. Hii itakuwa ni kupitia youtube.com/TaylorSwift kwenye mida ya 4pm PST / 7 EST Tarehe 13/8 siku ya Jumatatu ili kusikia habari kubwa kutoka kwa Taylor Swift na pia wewe kumuuliza maswali yako yoteee. Kwa kujiuliza... Ni habari gani kubwa anayotaka kuisema??? Labda tuhisi ni kutoka katika album yake itakayofuata... Jiandae na Taylor siku ya Jumatatu.
Angalia Taylor swift akitangaza hapo chini...

NONIN RAPA WA KENYA

Habari ni kwamba Kenyan Rapper/Singer amechukua nafasi ya Tina Kaggia katika kipindi cha asubuhi, yaani 'Breakfast Show' katika kituo cha radio cha 1FM. Nonini sasa atatangaza kipindi hicho na Marcus Olang' ambapo Tina Kaggia amehamia katika kipindi kingine katika radio hiyo.
       Wengine wanaweza kudhani Nonini ni mpya katika utangazaji wa Radio lakini aliwahi kufanya kazi kama Celebrity Radio Presenter katika kituo cha Radio cha YFM, ambayo kwa sasa inafahamika kama HOT 96.
       Nonini ni msanii aliyeshinda tuzo nyingi toka atoke kimuziki mwaka 2000 kutoka studio za Calif (Calif Records). Nonini ni mmoja wa wasanii waliotunga aina ya muziki wa Genge na sasa hivi anatambulika na Jamii ya Haki Miliki ya Muziki nchini Kenya.
Source: Kenyanlist


Wednesday, August 8, 2012

BMW X6

Anayesema Bongo muvi hailipi ni nani??Ijapokua kazi za wasanii zinaibwa, kidogo wanachopata kinaweza kuwafanya wabadilishe maisha yao.Swali kwa wewe mdau wa MUVI zetu za nyumbani!Hivi wewe unafikiri ni njiagani itatumika kukomesha wizi wa kazi za wasanii?

KWA WALE WAPENZI WA BONGO MUVI
 Chuchu Hans na Batuli, moja kati ya washiriki
Jinsi script ilivyokua inatendewa haki.
Vijana wakiwa sait
Mzigo uliokuwa ukisubiliwa kwa hamu na wadau wa tsnia ya movie bongo sasa unaingia mtaani tarehe sita mwezi ujao ni bonge la movie na wala si yakuikosa maana imejaa mafunzo ya kutosha kuhusu mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...